Auric

Jumatatu, 23 Septemba 2013

Introducing to you 'My Trip Travel & Tours'

I would like to introduce My Trip Travel & Tours LTD a recently established company in Dar es Salaam, Tanzania. We have an excellent team of highly experienced, motivated and dedicated staff.

We will be delighted to help you with any future travel plans you may have, whether it is a cruise, a holiday package, wildlife safaris, honeymoon packages, adventure holiday, your flights, or a short break— whatever you are looking for, we are here and ready to help.


As a comprehensive travel agency, we are the agent for all Local and International Flights. We book online and issue you with an Electronic Ticket.

If you have been looking or booking online recently, please give us a call before you do so again, as a company we do offer services that are of the highest standard and at extremely competitive rates — and this can be done over the telephone or by email. You will also be able to use our staff’s knowledge to help you find the perfect holiday.

We hope you will support My Trip Travel & Tours LTD and give us a call on +255 688 002000/ +255 776 944 444, email toinfo@mytriptraveltz.com, or drop in to our office at Royal Mirage Hotel Building, Ground Floor at Living stone/Amani Street tosee us.
We are looking forward to assisting you and hope you will contact us in case you need to utilize any of the services and expertise that our company provides.


We guarantee you high quality service.

Picha sita za muonekano wa jengo jipya la uwanja wa ndege wa Mwalimu Julius Nyerere (JNIA) baada ya ujenzi kukamilika

Harakati za maandalizi ya ujenzi wa jengo jipya (Terminal 3) la uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), zimekuwa zikiendelea polepole hali inayowatia shaka wadau wengi wa sekta hii ya usafiri wa anga. Kuanza kwa ujenzi wa jengo hilo ni jambo linalosubiriwa kwa hamu kubwa na wadau wa sekta ya usafiri wa anga kwani kukamilika kwa jengo hilo kunategemewa kuleta mabadiliko makubwa sana katika huduma zitolewazo na kuleta ufanisi mkubwa katika huduma za usafiri wa anga na hatimae kukuza uchumi wa nchi.

Hivi karibuni wataalamu na mafundi wa kampuni iliyopewa zabuni ya kujenga jengo hilo, kampuni ya BAM ya Uholanzi, walionekana wakifanya maandalizi ya mwanzo ya ujenzi huo ikiwa ni pamoja na kuzungushia uzio baadhi ya maeneo, upimaji wa ardhi na kubandika michoro yenye kuonesha jinsi taswira ya jengo hilo itakavyokuwa.

Mtandao wa Aviationtz umeshare picha zifuatazo zikionyesha maeneo mbalimbali ya jengo hilo pamoja njia za ndege.

Huu ni muonekano kwa upande wa nje ya jengo na nje ya uwanja.

Hapa ni mahali ambapo abiria watakuwa wakisubiri kabla ya kwenda kupanda ndege (Departure Lounge)
Muonekano wa ndani ya jengo

Jinsi patakavyoonekana kutokea angani

Muonekano wa jengo,njia za ndege na maegesho ya magari.

Upande wa maegesho ya ndege
Ujenzi wa jengo hilo umepangwa kufanyika kwa awamu mbili. Kukamilika kwa awamu ya kwanza kutawezesha uwanja huo kufikia uwezo wa abiria mil 3.5 kwa mwaka tofauti na jengo la sasa ambalo uwezo wake ni abiria mil 1.5 kwa mwaka. Awamu ya pili itaongeza uwezo huo hadi kufikia abiria mil 6 kwa mwaka. Baada ya kukamilika jengo hilo, jengo lililopo sasa (Terminal II) litatumika kwa shughuli za abiria wanaosafiri ndani ya Tanzania tu.

Chanzo: Aviationtz